Fainali za Kombe la Shirikisho maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) zinatarajiwa kufanyika kesho Mei 25, 2016 kwa kuzikutanisha timu za Young Africans na Azam FC; zote za Dar es Salaam katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Taifa jijini.

Sherehe za mchezo huo zitaanza rasmi saa 8.00 mchana kwa mchezo wa awali wa kuburudisha kuzikutanisha timu za soka za kituo cha Televisheni cha Azam ‘Azam Tv’ na wafanyakazi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kurushwa live na kituo hicho kilichotokea watazamaji wa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Viingilio katika mchezo huo itakuwa ni Sh 25,000 kwa VIP A wakati VIP B na C ni Sh 20,000 wakati majukwaa yenye viti vya rangi ya chungwa, mzunguko wenye viti vya rangi ya bluu na kijani ni Sh 5,000.

TFF inajivunia nyota wake kama Jemedari Said, Wilfred Kidao, Salum Madadi, Alfred Lucas, Danny Msangi, Michael Ngogo na Jonas Kiwia, lakini Meneja wa timu ya Wafanyakazi wa TFF, Eliud Mvella anasikitika kumkosa nyota wake Mwesigwa Selestine.

Azam Tv wanatamba na nyota wao waliopata kufanya kazi nje ya nchi katika vyombo vya kimataifa kama vile Charles Hilary, Tido Mhando, Yahaya Mohammed, Baruan Muhuza na Rhys aliyetajwa kwa jina moja.
Mbali ya burudani hiyo, pia Mwakilishi wa Azam Tv, Baruan Muhuza alisema kwamba mara baada ya mchezo huo utakaomalizika saa 9.00 alasiri, itafuata burudani ya wasanii mbalimbali ambao pia wataburudisha wakati wa mapumziko ya mchezo huo.

SOMA ZAIDI HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...