• Wawezeshwa vitendea kazi vyenye dhamani ya shilingi milioni tano.
Airtel Tanzania inaendeleza dhamira yake ya kuendelea kuwashika mkono vijana hapa nchini ambapo mwishoni mwa wiki hii kupitia mpango wake wa kutoa semina ya mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana ujulikanao kama Airtel FURSA Tunakuwezesha, uliweza kuchagua vijana wawili walioweza kuelezea na kuwakilisha changamoto wanazozipata katika biashara wanazozifanya mbele ya jopo la washauri ambao leo hii wamekabidhiwa vitendea kazi vyenye dhamani ya shilling milioni 5 ili kuweza kukabiliana na changamoto hizo.
Akizungumza wakati wa sherehe ya makabidhiano hayo, Meneja wa Airtel huduma kwa Jamii Hawa Bayumi alisema "baada ya kufanya mafunzo ya biashara ya ujasiriamali wiki chache zilizopita na kuweza kufikia vijana zaidi ya 300 jijini Dar Es Salaam waliojitokeza na kuzifahamu vyema FURSA zinazowazunguka ili kujitengenezea ajira na na uwezo wa kujenga fursa nyingine. Leo hii tupo hapa kuwawezesha hawa walioonyesha bidi zaidi”
“Na siku hiyo ilikuwa ni siku ya faraja kwani vijana waliweza kujifunza mambo mengi sana na mwisho wa siku waliweza kuelezea na kuwasilisha biashara zao mbele ya jopo la washauri na ulikuwa uamuzi mgumu sana lakini mwisho wa siku tuliweza kupata vijana wawili bora walioweza kushinda nyoyo za jopo la washauri hao, ambao leo hii tupo hapa kwajili ya kuwakabidhi vifaa vyao ili waweze kwenda kukabiliana na changamoto walizonazo katika biashara zao. "
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Stephen
Gimase (Kulia) ambaye ni miongoni wa vijana waliowezeshwa na mpango wa
Airtel FURSA “Tunakuwezesha” akiangalia vifaa alivyokabidhiwa na Airtel
FURSA kwa ajili ya kuboresha biashara yake ya kutengeneza mashine za
kutengenezea vifaranga vya kuku, Kushoto ni Meneja wa huduma za jamii wa
Airtel, Hawa Bayumi
Meneja
wa huduma za jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (2 Kushoto) akimkabidhi
Theresia Maliatabu (Kulia) ambaye ni miongoni wa vijana waliowezeshwa na
mpango wa Airtel FURSA “Tunakuwezesha” vifaa vyakuboresha biashara yake
ya uchoraji ikiwemo meza ya kuchorea na kompyuta ya kisasa. Kijana huyu
Aliyechaguliwa kutoka kwenye mafunzo ya biashara ya ujasiriamali ya
Airtel FURSA yaliyofanyika Dar es Salaam wiki chache zilizopita.
Akishuhudiwa na mama yake mzazi Judith Benedicto (Katikati) na mama
mkubwa Salome Benedicto (Kulia) pamoja na Afisa mauzo wa Airtel katika
hafla iliyofanyika Mbagala kuu, jijini Dar es Salaam.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...