Kocha Mkuu wa Yanga Hans Van De Pluijm 
akiwasabahi mashabiki wa timu ya Yanga.

Na Zainab Nyamka,
 Globu ya Jamii.
MABINGWA wa soka Ligi Kuu ya Bara wamewasili jijni wakitokea Angola katika mechi ya narudiano dhdi ya Espirance Sagdrada ya Angola.
Yanga ambayo imefuzu hatua makundi wamewasili mida ya saa nane na dakika 45 na mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa kocha wa timu hiyo Hans Van Pluijim amesema timu imefanya vizuri pamoja na figisu figisu ambazo wamefanyiwa.
Amesema anawapongeza viongozi wa Yanga kwa kupambana na hujuma lakini wamefanikiwa kuingia hatua ya makundi na wamejifunza mengi Angola ambapo watayafanyiwa kazi huku akiwapongeza wachezaji wake kwa juhudi walizoonyesha uwanjani kuhakikisha wanafuzu.
"Wachezaji wamefanya vizuri na wamejituma na kuhahakikisha wanavuka hatua hiyo na wamejituma sana nawapongeza na tumejifunza mengi sana Angola,"amesema Pluijm.
Amesema  kikosi kwa sasa hakina cha kupoteza kitaendeea na kambi kuhakikisha wanasonga mbele katika mashindano hayo lengo lao ni kuona wanafika hatua ya fainali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...