MAANDALIZI ya Ripoti ya pili ya Maendeleo ya Binadamu (THDR) inayotarajiwa kuzinduliwa Juni 2017 yamefikia katika ngazi ya mwisho ya ukusanyaji wa maoni ya kitaalamu katika mada mbalimbali zinazojadiliwa katika ripoti hiyo.

Maandalizi hayo yanayowezeshwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) kwa msaada wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na wadau wengine yanafanyika kwa mfumo wa warsha ya siku mbili jijini Dar es salaam, jana Jumatatu na

Katika warsha hiyo ya rasimu ya pili na ya mwisho kabla ya uhariri, inajadiliwa na wanazuoni kupitia mada 11 ambazo zitakuwapo katika taarifa hiyo ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2017.

Warsha hiyo ya siku mbili itatoa msingi wa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu nchini kwa kuangalia Sera ya hifadhi ya jamii katika muktadha wa mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania.

Miongoni mwa mada zilizojadiliwa jana baada ya ufunguzi wa kongamano hilo uliofanywa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida ni usambazaji wa maji kwa kuangalia sera, fedha na upatikanaji wake; elimu; sera ya jamii na mabadiliko ya kiuchumi; na hifadhi ya jamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akifungua warsha ya siku mbili iliyowakutanisha wanazuoni kuandaa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu Tanzania ya mwaka 2017 jijini Dar es Salaam. (Picha na Modewjiblog)

Pichani juu na chini ni sehemu ya washiriki wakiwasilisha maoni yao katika warsha ya rasimu ya pili na ya mwisho kabla ya uhariri, inayojadiliwa na wanazuoni hao kupitia mada 11 ambazo zitakuwapo katika taarifa ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2017.

Akifungua kongamano hilo Dkt. Kida aliwataka wadau wote kutambua kwamba kazi wanayoifanya ni ya muhimu sana kwa taifa kwani imekuwa chanzo cha upangaji wa mipango ya maendeleo na namna inavyostahili kuwa.

Alisema mpango wa pili wa maendeleo nchini kuelekea uchumi wa kati umechukua fikra na falsafa nyingi kutoka katika taarifa ya Maendeleo ya Binadamu iliyofanyiwa mwaka 2014 na kuzinduliwa mwaka 2015.

Mpango wa maendeleo wa pili wa miaka mitano uliozinduliwa wiki iliyopita umetumia vionjo vingi kutoka katika ripoti iliyopita na hivyo ni vyema wadau wakachangia mada hizo na kuzipa uhai mkubwa zaidi kwa manufaa ya Ripoti ijayo alisema Dkt. Kida.

Aidha aliwataka wahusika wote kuwa karibu na ESRF wakati wa uandishi wa mwisho ya ripoti hiyo baada ya kumalizika kwa kongamano hilo.
Mtafiti mwandamizi mshiriki na Mshauri wa kiufundi wa mradi wa THDR, Marc Wuyts akizungumzia mada ya uhusiano wa sera ya jamii na mabadiliko ya kiuchumi katika warsha hiyo ya siku mbili inayoendelea jijini Dar esSalaam.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...