Assalaam alaykum wanajamii.
Leo hii tarehe 13/06/2016 sisi NGURUMO ZA SIMBA WHATSAP GROUP tumetimiza mwaka mmoja toka kuanzishwa rasmi tarehe 13/06/2015.
NGURUMO ZA SIMBA ni kundi la mashabiki,wapenzi na wanachama wa Simba ambao wameamua kuungana na kutengeneza kundi moja kubwa kwa kazi ya kujitolea kwa ajili ya Simba SC.
Kundi letu ambalo leo hii linatimiza mwaka mmoja toka kuundwa kwake,lipo mstari wa mbele kuhakikisha kwamba sisi washabiki,wapenzi na wanachama tunazidi kutoa elimu kwa wale wote ambao hawana uanachama wa Simba SC kufahamu faida za kuwa mwanachama ambazo ni pamoja na kuongeza mapato kupitia malipo ya ada ya mwaka ya Simba SC.
Tayari mpaka sasa wapenzi na mashabiki wengi walioungana nasi wamepata uanachama wa Simba SC.
Tupo mstari wa mbele kuhakikisha tunawasaidia wapenzi,washabiki na wanachama kuwa na Umoja ambao ni muendelezo wa falsafa ya SIMBA NGUVU MOJA.
NGURUMO ZA SIMBA pia imejikita kuhakikisha wana Simba sisi wenyewe kushirikiana katika furaha ama huzuni.
Tunaendelea kuwaambia wana Simba wote duniani kuwa na subira kipindi hiki kigumu na tuendelee kuwa na ushirikiano mwema na viongozi wetu waliopo madarakani na tuwape ushahuri wa msingi ambao utakuja kutuletea mafanikio msimu unaokuja wa mwaka 2016/2017.
Simba nguvu moja.
HAPPY BIRTHDAY NGURUMO ZA SIMBA.
Imetolewa na:
DAWATI LA NGURUMO ZA SIMBA.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...