Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe akimkabidhi Mratibu Mkuu wa ICGLR, Balozi Samuel Shilukindo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje (Mwenyekiti) vitendea kazi wakati akizindua Kamati ya Kimataifa ya Kusimamia Utekelezaji wa Mpango wa ICGLR Tanzania jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (mbele) na kulia kwake aliyesimama ni Mratibu Mkuu wa ICGLR, Balozi Samuel Shilukindo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje akisoma hotuba wakati wa uzinduzi na wengine katika picha ni wanakamati.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (mbele) na wajumbe wa kamati hiyo wakimsikiliza Kaimu Kamishna wa Madini Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ally Samaje (aliyesimama) akitoa mada katika uzinduzi uliofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe wa nne kutoka kulia akiwa pamoja na Kamati ya Kimataifa ya Kusimamia Utekelezaji wa Mpango wa ICGLR Tanzania na Wajumbe kutoka Wizara ya Nishati na Madini wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza uzinduzi wa Kamati hiyo.

Na Rhoda James

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia madini Profesa James Mdoe kwa Niaba ya Katibu Mkuu, Profesa Justin Ntalikwa tarehe 22 Juni, 2016 alizindua Kamati ya Kimataifa ya Kutekeleza Mpango ujulikanao kama International Conference on the Great Lakes Regional Initiative Against Illegal Exploration of Natural Resources (ICGLK- RINR) katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dar es Salaam.

Profesa Mdoe alisema kuwa lengo la Mpango wa ICGLR- RINR ni kuweka mfumo wa usimamizi wa uchimbaji, uchenjuaji, usafirishaji na uuzaji wa madini ili kuhakikisha kuwa shughuli hizo zinafanywa kihalali na hazitumiwi na vikundi au watu wanaohusika katika kuendeleza migogoro na vita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...