Katika miaka ya hivi karibuni ufugaji wa kuku umekua kwa kiasi kikubwa na kuwa mtaji mkuu wa wajasiriamali wadogo na wakubwa katika kujiingizia kipato.

Mkurugenzi wa Kuku Project Mary David
Hata hivyo ufugaji wa kuku nao umekuwa ukienda kwa wakati kutokana na ukuaji wa teknolojia. Moja ya teknolojia hizo ni mashine za kutotoleshea vifaranga kitaalamu; ‘incubator’.

Mary David maarufu kama ‘Mama Kuku’ ni Mkurugenzi wa Kuku Project Tanzania, ambaye pia ni msambazaji wa mashine za kisasa za Incubator, yeye anasema kuwa mashine hizo zimekuwa mkombozi kwa wafugaji wa kuku nchini kwa kuwa huuzwa kwa bei rahisi inayoendana na mahitaji ya mfugaji mwenyewe.“Incubator zetu ni za bei tofauti kuanzia shilingi laki nne na nusu ambazo zina uwezo wa kubeba mayai arobaini na nane na kubwa kabisa ambayo hubeba mayai elfu kumi na tisa mia saba kumi na mbili ambayo huuzwa kwa shilingi milioni ishirini,” anasema Bi. Mary.

Mbali na hayo, Bi. Mary anasema kuwa incubator hizo huwa na uwezo wa kutumia umeme, nishati ya jua na pia kuhifadhi umeme kwa masaa sita baada ya umeme  kukatika ambapo pia mtumiaji atapata fursa ya kuelekezwa jinsi ya utumiaji wake huku mashine hizo zikiwa na waranti ya mwaka mzima.


Kwa maelezo zaidi na jinsi ya kununua Incubator fika DAR ES SALAAM,MAGOMENI MWEMBE CHAI,NYUMA YA KANISA LA  WASABATO. SIMU : +255 653 691 138+255 715 908 307,+255 678 226 988






Kujua zaidi Like Page yao kwa kubofya hapa :


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...