Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili, Maj. Gen.
Gaudence Milanzi (katikati) akisaini hati ya makubaliano kati ya Serikali ya
Tanzania na Zambia, jijini Dar es Salaam jana kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za udhibiti wa usafirishaji wa
mazao ya misitu hususan magogo katika mipaka ya nchi hizo mbili. Wanaoshuhudia kulia ni
Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili, Gladynes Mkamba na
Kaimu Mtendaji Mkuu TFS, Richard Kamwenda (kushoto). Waliosimama kulia ni
Mwanasheria wa TFS, David Mung’ong’o na Mwanasheria wa Wizara ya Maliasili, Stephen
Mwamasenjele.
Katibu Mkuu
Wizara ya Ardhi, Maliasili na Hifadhi ya Mazingira wa Serikali ya Zambia,
Trevor Kaunda akisaini makubaliano hayo.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili, Maj. Gen.
Gaudence Milanzi (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Maliasili na Hifadhi
ya Mazingira wa Serikali ya Zambia, Trevor Kaunda wakibadilishana hati ya makubaliano
waliyosaini kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za udhibiti wa usafirishaji wa mazao
ya misitu hususani magogo katika mipaka ya nchi hizo.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili, Maj. Gen.
Gaudence Milanzi (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Maliasili na Hifadhi
ya Mazingira wa Serikali ya Zambia, Trevor Kaunda wakiangalia sehemu ya magogo
yaliyokamatwa hivi karibuni katika bandari ya Dar es Salaam kutoka nchini
Zambia na DRC. Makatibu Wakuu hao wamesaini makubaliano ya kukabiliana na
changamoto za udhibiti wa usafirishaji wa mazao ya misitu hususani
magogo kwenye mipaka wa nchi hizo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...