Na Abdulaziz Video,Lindi

Madiwani wa Halmashauri za Wilaya ya Kilwa na Ruangwa Mkoani Lindi Zimeanza Utekelezaji wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID) kwa Kupatiwa Mafunzo ya Siku 4 na Kuratibiwa na Tamisemi

Kuanza kwa Hatua Hiyo kunafuatia kumalizika kwa Mafunzo kwa Watendaji wa Halmshauri 6 Za Mkoa wa Lindi juu ya Namna ya Kushiriki na Kutekeleza Mradi huo Utakaotekelezwa kwa Kipindi cha Miaka 5 Ijayo

Akifungua Mafunzo hayo,Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi amezitaka Halmashauri Hizo Kufuatilia kwa Umakini Mafunzo yanayotolewa na wakufunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa Hombolo ili Kupata Uelewa Juu ya Uendeshaji wa Halmashauri

‘’ Madiwani ni kiungo muhimu baina ya serikali na watendaji wa serikali madiwani Musipokuwa Vizuri Mtaburuzwa na Watendaji hususan katika Utendaji na Utekelezaji wa Miradi hasa Ikiwa Diwani Una Tabia ya Kuomba omba na Kukopa kwa Mkurugenzi au Mkuu wa Idara Lazima Mjipime Nyie Ndio wamiliki wa Halmashauri au hamjijui?’’Alimalizia Zambi
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Akitoa Hotuba yake ya Ufunguzi ambapo Pia Aliwataka Madiwani Kuacha Siasa katika Kutekeleza Maendeleo ya Halmashauri zao,Kulia ni Mkurugenzi wa Shughuli za Mikoa Mradi wa Ps,Bw Conrad Mbuya
Madiwani wa Ruangwa Pamoja Na Mwandishi wa Vikao Vya Baraza la Madiwani Ruangwa,Bahati kasabano (Kulia)wakifuatilia mafunzo hayo
Afisa Mshauri wa Masuala ya Utawala Bora PS3, Nazar Sola akitoa Elimu kwa Madiwani juu ya Utekelezaji wa Mifumo ya Utendaji na Utoaji Huduma
Baadhi ya madiwani na watendaji wa halmashauri za Kilwa na Ruangwa Mkoani Lindi wakifuatilia jambo katika semina Elekezi ya Kujenga Uelewa kwa Halmashauri kupitia Mradi kuimarisha Uwezo wa Kutoa Huduma kwa Jamii Chini ya Utekelezaji wa Mradi wa PS3 Unaofadhiliwa na USAID.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...