Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala Bi. Tabu Shaibu akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu Ulinzi na Usalama wa Mtoto kuelekea Siku ya Mtoto wa Afrika inayoadhimishwa Juni 16 kila mwaka. Kushoto ni Afisa Ustawi wa Amana One Stop Centre Bw. Sophian Mndolwa na kulia ni Mratibu wa Timu ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto Manispaa ya Ilala Bw. Waziri Nashiri.
Mratibu wa Timu ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto Manispaa ya Ilala Bw. Waziri Nashiri (kushoto) akiwaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mipango ya Manispaa hiyo katika kuwasaidia watoto walio kwenye mazingira hatarishi. Kulia ni Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala Bi. Tabu Shaibu na katikati ni Afisa Ustawi wa Amana One Stop Centre Bw. Sophian Mndolwa.
Afisa Ustawi wa Amana One Stop Centre Bw. Sophian Mndolwa akieleza kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu taratibu za kufuata ili kupata huduma katika kituo cha Amana One Stop Centre ambacho kinahusika na kutoa msaada kwa watoto wanaofanyiwa ukatili wa aina mbalimbali. Kulia ni Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala Bi. Tabu Shaibu.Picha na Fatma Salum (MAELEZO)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...