Benjamin Sawe -Maelezo
Dar es Salaam

Amani ni msingi wa maendeleo na hivyo ni muhimu kwa nchi yoyote duniani.Bila amani,nchi haiwezi kufanya shughuli za maendeleo hata pale ambapo maendeleo yameshapatikana,huweza kuvurugwa endapo amani itatoweke katika nchi.

Nchi ambazo kwa miaka ya hivi karibuni zimejitaidi kupiga hatua za maendeleo na zinaendelea kufanya jitiada kuhakikisha kuwa zinapiga hatua kubwa zaidi ya maendeleo kwa faida ya wananchi wote,jitiada hizo pia,kwa baadhi ya nchi zimeathiriwa na migogoro.

Matokeo ya migogoro hiyo ni mamilioni ya waafrika wasio na hatia kupoteza maisha yao na mamilioni zaidi kujeruhiwa.Pia mamilioni ya wanawake na watoto kupatwa shida kubwa na baadhi ya watu kukimbia nchi zao na kukimbilia nchi za jirani katika kuokoa maisha yao hivyo kujikuta wakiishi maisha ya dhiki nje ya nchi yao.

Takwimu zinaonyesha kuwa mwaka 2009,Afrika ilikuwa na wakimbizi milioni 3 ambayo ni asilimia 20 ya wakimbizi wapatao milioni 10.5 duniani.Aidha,Afrika inakisiwa kuwa ina watu milioni kumi na mojana laki sita ambao wamelezimika kuhama makazi yao kwa ajili ya vita

Migogoro migogoro huwa kikwazo kikubwa cha shughuli za maendeleo siyo tu kwa watu binafsi bali pia kwa taifa.Fedha ambazo zingeweza kuelekezwa kwenye huduma muhimu ya jamii kama afya,elimu,maji ni fedha ambazo huelekezwa katika manunuzi ya silaa.

Inakadiriwa kuwa hasara ya kiuchumi inakadiriwa kuwa wastani wa dola bilioni kumi na nane kwa kila mwaka sababu ya migogoro.

Hali hii ya migogoro katika bara la Afrika imelifanya bara hili kujulikana kama bara la mapigano jambo ambalo ni dhahiri linasikitisha hivyo hatuna budi kuondokana na hali hiyo ya migogoro na kuwa bara huru lisilo na migogoro. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 15, 2016

    Ni vizuri migogoro inapojitokeza ishughulikiwe kuitatua kwa mazungumzo yanayolenga kusuluhisha kiini cha migogoro pale inapojitokeza badala ya kungoja mpaka hali inapokuwa mbaya, maafa kutokea, wananchi kuumia, na nchi kudhurika.

    ReplyDelete
  2. mwandishi maarufu aliwahi kusema ukiiangalia ramani ya Afrika imekaa kama pistol ukiamua kishikio kiwe somalia kifyatulio kinakua DRC NA UKIAMUA KISHIKIO KIWE DRC KIFYATUIAO KINAAKUA KWENYE PEMBE YA AFRIKA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...