Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii NSSF limefanya semina na kuzindua mpango wa kuwaandikisha maadereva wa Bodaboda Mkoani Dodoma, Mpango huo ulifanywa kwa ushirikiano wa Manispaa ya Mji wa Dodoma, VETA , Trafiki Mkoa na NSSF umezinduliwa na Waziri wa Nchi , Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira,Vijana na Watu wenye Ulemavu Jenista Mhagama.

Pamoja na Uzinduzi wa Uandikishaji Waziri Jenista Mhagama aliwapatia Vifaa vya Usalama Madereva hao wa BodaBoda Mkoani Dodoma vifaa hivyo ni Kofia ya Usalama na Kikoti Maalumu cha Usalama ambavyo vimeandikwa Namba kulingana na Kituo cha Bodaboda Wanachofanyia Kazi. Pia Waziri amezindua mfumo wa kuvipa namba na kuviweka alama Vibao vituo vyote vya Bodaboda mkoani Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof. Godius Kahyarara akiongea na Madereva wa Bodaboda (hawapo pichani) wakati wa Uzinduzi wa rasmi wa Kampeni ya Kuandikisha Madereva wa Bodaboda Mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi , Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira,Vijana na Watu wenye Ulemavu Jenista Mhagama akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Mpango wa kuwaandikisha madereva wa Bodaboda Mkoani Dodoma.

Meneja wa NSSF Mkoa wa Dodoma Rehema Chuma akitoa elimu kwa Madereva wa Bodaboda wa Mkoa wa Dodoma waliouzulia zoezi la uzinduzi wa kampeni rasmi ya kuwatambua na kuwaandikisha NSSF madereva wa Bodaboda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...