
Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (wa kwanza kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Profesa Tolly Mbwete (katikati) hati ya mauzo ya hisa asilimia 35 za Kampuni ya Bharti Airtel Afrika. Serikali imezinunua rasmi hisa za kampuni hiyo ndani ya TTCL ambapo leo wamesaini mkataba wa mauziano wa hisa hizo. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria akishuhudia.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (kushoto waliokaa) akitiliana saini na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu) kwenye hafla ya kusaini mkataba wa mauziano. Serikali leo imezinunua rasmi hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel Afrika ndani ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL). Nyuma waliosimama ni viongozi mbalimbali walioshuhudia tukio hilo.

Msajili wa Hazina, Laurence Mafuru (mwenye tai ya bluu) akionesha hati ya mauziano ya hisa. Serikali leo imezinunua rasmi hisa asilimia 35 za kampuni ya Bharti Airtel Afrika ndani ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), ambapo sasa inakuwa ikiimiliki TTCL kwa asilimia 100. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Bharti Airtel Afrika, Christian De Faria (mwenye tai nyekundu) akiwa kwenye hafla ya kusaini mkataba wa mauziano hayo. Nyuma waliosimama ni viongozi mbalimbali wa TTCL na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano walioshuhudia tukio hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...