Na Geofrey Chambua
#1.TEMBO unayemjua wewe kwa wastani ana uzito wa kilogramu elfu kumi kwenda mbele (Hapa namuongelea tembo mkubwa)  Tembo pamoja na ukubwa wake akitembea hana kishindo kabisa miguu yake kwa chini ni kama ina sponge hivi.

#2. Wakati mwanamke anabeba ujauzito kwa kipindi cha miezi tisa, TEMBO mkubwa wa kike anabeba ujauzito kwa jumla ya miaka miwili yaani miezi ishirini na minne kabla hajazaa.
#3. Ukimwondoa mwanadamu ambaye ana KIDEVU, Tembo ndiye mnyama mwinginbe  ambaye pia anacho kidevu…..
#4. Tembo anao uwezo wa kumsikia Tembo mwenzake akilia kutoka umbali wa kilometa tano….Tembo hana uwezo mkubwa wa kutambua vitu kwa kuona. hutegemea zaidi pua na masikio kuweza kufanikisha shughuli zake. kutokana na hali hiyo, mara nyingi ukiwa porini unashauriwa kumpiga picha tembo BILA ya kutumia flash. hii inatoka na kwamba, endapo utatumia flash wakati unampiga picha, tembo atajenga hisia ya kutoelewa nini kimetokea. kwa kifupi hataweza kutofautisha kama ni kitu cha kawaida au ni hatari. katika mazingira haya, huanza ku-charge kuelekea upande ule ambao mwanga
 #5. Ni Tembo wa Afrika pekee mwenye uwezo wa kutofautisha kabila, jinsia na umri wa mwanadamu. Ikiwa jana alijeruhiwa na mtu anayezungumza kiingereza, akisikia kiingereza anakumbuka upesi…
#6. Takribani Tembo mia moja huuwawa kila siku kwa sababu ya pembe zao….
#7. Kila mnyama kuna kitu anakiogopa sana, lakini ni ajabu sana kwa Tembo ambaye anamuogopa nyuki kuliko kitu chochote.
#8. Tembo mkubwa na mzito kupita wote anapatikana Afrika…
#9. Ikiwa mwanadamu hulala walau masaa nane kwa siku, kwa Tembo ni tofauti… Tembo hulala masaa mawili hadi matatu kwa siku!!
#10. Kuhusiana na mambo ya kula na kunywa… Tembo mkubwa huitaji walau kilo mia tatu za chakula na maji lita 160 kwa siku!!! Kama unahitaji kumfuga ujiandae……
11. Tembo anategemea sana uwezo wake wa kunusa ili kuweza kutambua mazingira aliyopo na vitu vinavyomzunguka. Sambamba na harufu, tembo pia ana uwezo mkubwa wa kusikia kupitia masikio yake makubwa (by the way, tembo porini huitwa Masikio).
12 Tembo ana fanya mapenzi kwa masaa 12; masaa 6 ya mwanzo anamuandaa mwenzi wake na 6yanayobaki ndio shughuli yenyewe na hiyo ni ile raundi ya kwanza.
13 Tembo dume huwa na wanawake wawili mpaka wanne
14. Akipiga bao tembo dume manii zake ni ujazo wa lita tano

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 11, 2016

    Tanzania inaongoza kwa mauaji ya tembo. Biashara haramu ya meno yake ni ya tatu duniani kifaida ukiacha mbili za mwanzo ambazo ni madawa ya kulevya na silaha. Wachina ndio wanunuzi wakubwa wa meno ya tembo. Serikali isipochukua hatua kuzuia mzunguko wote wa hii biashara yawezekana miaka michache ijayo hakutakuwa na tembo kabisa Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...