Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dr. Hamisi Kigwangalla ( Mb) akizungumza kwa niaba ya serikali kuhusu mafanikio na changamoto ambazo serikali imekuwa ikikabiliana nazo dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ni katika mkutano wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu ukimwi unaoendelea hapa Umoja wa Mataifa, Naibu Waziri anaongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu.
Naibu Waziri Mhe. Dr. Hamisi Kingwangalla akiwa katika picha ya pamoja mbele ya bendera ya Tanzania na sehemu ya ujumbe wa Tanzania unaoshiriki mkutano wa ngazi ya juu kuhusu ukimwi, mara tu baada ya kusoma hotuba yake katika Ukumbi Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambapo mkutano huu wa siku unafanyika.
Na Mwandishi Maalum, New York
Mkutano wa nganzi ya juu kuhusu ukimwi jana ( alhamis) uliingia katika siku yake ya pili ambapo viongozi mbalimbali wakiwamo Mawaziri na Naibu waziri wanaohusika na masuala ya afya wameendelea kuelezea nini ambacho nchi zao zinatekeleza katika kukabili na kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vinavyo sababisha ukimwi pamoja na huduma wanazopatiwa watu ambao wamekwisha kuathirika na kuugua.
Mmoja ya nchi ambayo iliwasilisha mafanikio, changamoto na mwelekeo wa baadaye katika kukabiliana na janga la ugonjwa wa ukimwi, ugonjwa ambao jumuiya ya kimataifa umejiweka lengo la kuutokomeza ifikapo mwaka 2030 ili kuwa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
SOMA ZAIDI HAPA
SOMA ZAIDI HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...