Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

KIKOSI cha Yanga kilichopo nchini Uturuki hivi sasa, kimeendelea kujifua usiku ikiwa ni moja ya mkakati wa kocha mkuu wa timu hiyo Hans Van De Pluijm katika kuelekea mchezo wao dhidi ya Mo Bejala unaotarajiwa kuchezwa usiku nchini Algeria.

Pluijm ameonekana kutumia njia hiyo ikiwa ni pamoja na kuwapa mbinu mbalimbali kwani ameweka wazi kuwa anajua aina zote za hujuma zinazotumiwa na mataifa ya kiarabu. 

Yanga ipo nchini Uturuki ikijiandaa na mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Mo bejala ambapo ikishamaliza mchezo huo itarejea tena Uturuki na kumalizia kambi hiyo kabla ya kuja kuvaana na TP Mazembe Julai 28 jijini Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa Timu ya Yanga, Hans Van De Pluijm akitoa maelekezo kwa wachezaji wake, wakati wa Mazoezi yao ya Usiku huko nchini Uturuki.
Wachezaji wa Yanga wakimsikiliza mwalimu wao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...