Hata mbuyu ulianza kama uyoga. Na Bw. Adam wa Adam Auto Garage ya mjini Tunduma mkoani Songwe amedhihirisha hilo kwa kuunda helikopta inayotumia injini ya gari ambayo anasema anatarajia kuirusha siku Mwenge wa Uhuru utapofika mjini hapo. Picha za ubunifu huu zimesambaa kwenye mitandao ya jamii ila cha ajabu hakuna mamlaka iliyoshituka.
Bw. Adam akipongezwa kwa ubunifu wake ambao mamlaka husika zinaombwa kwenda na kuangalia namna ya kutumia kipaji hiki cha aina yake kwa maendeleo ya Taifa
Wananchi wakiishanga helikopta ya Adam Auto Garage mjini Tunduma
Bw. Adam na timu yake







The mdudu, Asante sana ndugu Adam hongera sana tena sana mimi nadhani wakati umefika sasa wa kutambua vipaji kama hivi serikali muwape support ili wazi tengeneze nyingi sana kisha wazisambaze kwenye mahosipital na police
ReplyDeleteNi wakati sasa usafiri huu uwe ni wa kawaida hapa nchimi. Kuwe na helikopta za Kibamba to Posta, Tegeta to Posta, Korogwe to Tanga, Segera to Chalinze ... ili kupunguza muda wa safari na kuondoa msongamano barabarani. Wajitokeze wawekezaji kuchukuwa fursa hii kwa kuwatumia vijana kama hawa
ReplyDeleteHuyu na yule wa holkopta ya arusha na wataalamu wa mifumo ya umeme..mafundi redio na ICT wakutane waone jinsi ya kuiboresha kwa kutumia teknolojia za kisasa. Hongera.
ReplyDeleteNdugu Adam hongera. Tz INA wanasayansi wabunifu wengi trend inaonyesha tu. Everything is possible viongozi has a Mkuu Wa mkoa na wilaya mbeya where r you guys. You should be proud. Mbeya tech university join hands with this group. This is one shovel ready project to jump in and finance. Ahhh . Mr Adam post your phone number. I am from mbeya I will visit you.
ReplyDeletePongezi kwake.
ReplyDeleteHow does the law protect this kind of innovation? it is time for the country to take these kind of innovation seriously. Hata wale watengeneza magobore ya kienyeji wachukuliwe na Jeshi kwa manufaa ya taifa.
ReplyDeleteHongera sana Mr Adam
ReplyDeleteUhakika taifa linahitaji watu kama nyie ilikuendeleza ukombozi wa taifa katika swali Zima la viwanda ili kufikia uchumi wa Kati
Sasa ni wakati serikali iwashike mkono wa kama akina Adam kwa kuwa patia fedha, kuandaa mazingira rafiki, na kuwaongezea ujuzi ikiwezekana.