NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemain Jaffo amesema kuwa fursa za elimu ni nyingi katika vyuo vya nje ya nchi na gharama zake ni nafuu.

Jaffo ameyasema hayo wakati wa maonesho ya biashara ya Kimataifa katika Viwanja vya Mwalimu J.K Nyerere (Sabasaba) katika banda la Global Education Link (GEL), amewataka Watanzania kutumia maonyesho ya Sabasaba kuwa ni kipindi muafaka kupata mambo mengi kwa wakati mmoja likiwamo suala la elimu katika vyuo vya nje.

Jaffo amesema kuwa, maonesho ya sabasaba ni kipindi pekee kwa taasisi mbalimbali na huduma zake zinatolewa bure.Aidha amesema kuwa wazazi wanaotaka kuwasomesha watoto wao katika vyuo vya nje ya nchi kwa gharama nafuu watumie fursa hiyo kupita katika banda la Global Education Link (GEL) watapata taarifa mbalimbali.

‘’Serikali ya awamu ya tano ya Rais Dk. John Pombe Magufuli imejipanga hivyo kama wasaidizi wake lazima tujipange kuhakikisha kwamba tuangalie jinsi ya kubadilika kwa kasi na kubadilika huko kwa kwa kasi lazima tuhakikishe tuna teknolojia yakutosha kabisa kwanza kiushindani, tuanzishe vitu ambavyo vitakuwa na soko kubwa”amesema .
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Education link (GEL), Abdulmalik S.Mollel amesema kuwa vijana wanaopitia kampuni yao hata baada ya kupata udahili na kwenda masomoni nje ya nchi, wana utaratibu wa kufuatiliwa maendeleo yao ili mzazi aweze kuona thamani ya fedha anayetoa kwa kusomesha mtoto nje ya nchi.

Mollel amesema kuwa vyuo vya nje wanavyokwenda wanafunzi kuna wawakilishi wanaofanya kazi moja kwa moja na GEL ya kufatilia mienendo ya wanafunzi wao kwa kipindi chote wanachosoma na taarifa zao zinatumwa na kisha mzazi kupewa taarifa za maendeleo ya mtoto.

Amesema kuwa watoto wanaokwenda kusoma vyuo vya nje vinatambuliwa na TCU na vinatambuliwa na bodi za nchi husika ili kuweza kumsaidia mtoto kuwa na uhakika wa elimu na utaalam aliyopata katika vyuo hivyo.

Global Education Link (GEL) inaangalia hali ya uchumi wa ndani kuwa mzazi anaweza kumudu gharama hizo na hakuna tofauti na vyuo vya ndani.Anasema mtoto anayesoma nje wanaangaliwa kwa kila namna kuanzia ili kumuondolea mzazi usumbufu.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Education link (GEL), Abdulmalik S.Mollel  akizungumza jambo na  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemain Jaffo alipokuwa akiagana nae mara baada ya kulitembelea banda hilo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...