Chama
Cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA),kimepokea kwa masikitiko
makubwa taarifa za msiba wa mwanachama wake,Elizaberth Mayemba
kilichotokea jana jioni huko nyumbani kwake Tabata kwa Swai.
TASWA imestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na kifo hiki cha Elizaberth ambaye mchango wake katika tasnia ya habari za michezo bado ulikuwa unahitajika sana.
Waandishi wa Habari za michezo wataendelea kumkumbuka Elizaberth kutokana na ucheshi,kujituma na uwajibikaji katika kufanikisha kazi zake na kuwa mfano kwa waandishi chipukizi.
TASWA inatoa pole kwa familia ya marehemu, marafiki na waandishi wote wa habari na kuwatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu.
Mwenyezi Mungu aipumzishe mahala pema peponi roho ya marehemu. TASWA ipo pamoja na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.
Juma Pinto
Mwemyekiti TASWA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...