Ofisa anayeshughulikia uangalizi wa Gridi katika Kituo cha kupoza umeme cha Iringa, John Havie, akimwonesha Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (kulia kwa John) namna anavyoongoza mitambo kupitia chumba maalum cha uangalizi (control room).
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (kulia) akimweleza jambo Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto (kushoto) walipokutana katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakati wa ziara ya Naibu Waziri kukagua miradi ya umeme mkoani humo hivi karibuni.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (wa tatu kutoka kushoto), akitoa maagizo kwa baadhi ya maofisa wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), wanaosimamia Bwawa la Maji la Mtera mkoani Iringa, alipotembelea Bwawa hilo ambalo maji yake hutumika kuzalisha umeme, akiwa katika ziara kukagua miradi ya umeme hivi karibuni.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...