Huu
ni Muendelezo wa Matukio Madogo Madogo yanayo endelea Kujitokeza katika
eneo la Mafiati Mataa Jijini Mbeya ambapo ndipo Sehemu pekee kati ya
Sehemu zote kwa Jiji zima kuwekwa Taa za kuongozea Magari na watembea
kwa Miguu kwa Mkoa mzima wa Mbeya kiukweli hapa ndipo ambapo pamepewe
kipaumbele
hicho cha kuwekewa Taa za kuongozea Magari na Watembea kwa Miguu,
Lakini cha kushangaza zaidi licha ya eneo hilo kupewe kipaombelele
kumekuwa na Vijipu Upele vingi ambavyo vinajitokeza mara kwa mara katika
eneo hilo ikiwemo hili la Taa moja Kupigwa Ngwala na Gari na
kutelekezwa kama uionavyo hapo katika Taswira ikiwa na Mmoja wa watembea
kwa Miguu akisubiri Taa hiyo iweze kumuongoza lakini hali ya kuwa Taa
hiyo ikiwa hoi Bin Taabani kutokana na kupokea Ngwala na Gari ambayo
hatukuweza Kuifahamu.
Kichwa
cha Taa hiyo Mpya iliyo wekwa hivi karibuni kuajili ya kuongozea
Wananchi watumiao Barabara hiyo ikiwa katika Uso wa simanzi Kando kando
ya Eneo hilo la Mafiati Mataa Jijini Mbeya..
Mmoja
kati ya watumiaji wa Barabara hiyo akisubiri Msaada wa Mbinu nyengine
ya kumuwezesha kuvuka Barabara kutokana na kumsubiri Muongozaji wake
alie Pigwa Ngwala bila mafanikio.
PICHA NA MR.PENGO MMG.
Trafiki wako wapi?, na hiyo ni kazi yao ya kwanza. Kuhakikisha watembea kwa mguu na vivuko vyao wako salama.
ReplyDeleteHuwa nasikutishwa sana tena sana jinsi madereva wazembe wanavyo gonga alama za usalama barabarani bila kuchukuliwa hatua. Napendekeza faini iwe kubwa mno. Dereva yeyote akigonga taa za barabarani au alama yoyote..atozwe faini kubwa. Hii kazi wapatieni wananchi. Gari ikigonga mtu yeyote atakaye toa taarifa apewe zawadi kama motisha.
ReplyDelete