Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir akitoa Nasaha katika futari Maalum iliyoandaliwa na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ambapo mufti mkuu aliwataka waislam kutojihusisha na matendo ya Kigaidi kwani hayaendani na maelekezo na mafundisho ya Allah.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa neno la shukrani kwa wageni waliojumuika kwenye futari aliyoiandaa nyumbani Oysterbay jijini Dar es Salaam kwake ambapo aliwataka Watanzania kudumisha mani na kuishi kwa upendo

Waalikwa kwenye Futari ilyoandaliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakiswali muda mfupi kabla ya kufuturu.

Sehemu ya Wageni waliohudhuria

Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya amani Sheikh Alhad Mussa akizungumza na waalikwa kwenye futari iliyoandaliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Padri John Solomon akitoa salaam za Kamati ya Amani wakati wa futari iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...