Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa mashujaa waliojitoa kwa uzalendo kupigania Tanzania hawana budi kukumbukwa kutokana na kujitoa kwao ili Tanzania isitawaliwe na wakoloni.

Makonda ameyasema hayo leo katika maadhimisho ya siku ya Mashujaa katika Mkoa wa Dar es Salaam yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, amesema kuwa mashujaa hao walifanya ukombozi kwa uzalendo bila kuangalia dini zao na makabila yao.

Makonda amesema kuwa kila mtu lazima ajiulize juu mashujaa katika kufanya kazi katika kungalia kutenda haki pamoja na uzalendo kwa masilahi ya taifa.

Amesema kuwa amani iliyopo nchini imetokana na watu kuwa wazalendo katika kupigania nchi yao na hawakuangalia kupoteza maisha au familia zao.

Aidha amesema kuwa watanzania wanatakiwa kuwa wazalendo na nchi bila kuangalia vyama wanavyotoka au kabila kutokana na umoja uliojengwa na mashujaa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiweka Ngao kwenye Mnara uliopo Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuwakumbuka Mashujaa waliopigana vita hapa nchini. Siku ya Mashujaa hufanyika Julai 25 kila mwaka.
 Askali wakitoa heshima wakati wa sherehe za kumbukumbu ya mashujaa ambayo imefanyika katika viwanja vya mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali jijini Dar es Salaam leo wakati wa sherehe za kuwakumbuka mashujaa waliopigana vita hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...