Mkuu mpya wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Nyabaganga Taraba
akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilayani
humo leo wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi. Katika hafla hiyo,
Taraba aliwataka watendaji wa wilaya hiyo kujituma kufanya kazi kwa
uadilifu, ushirikiano pamoja na kuwa waadilifu katika kuwatumika
wananchi.
Aidha, alimpongeza Mkuu wa wilaya hiyo aliyestaafu, Hawa Ngh’umbi kwa
utendaji wake huku akiahidi kuendelea kuchota hekima zake.
Mkuu wa Wilaya mstaafu, Hawa Ngh’umbi akitoa neno la shukrani kwa
wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani humo wakati akiagwa
baada ya kustaafu.
Mkuu wa wilaya aliyemaliza muda wake, Hawa Ngh’umbi (kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Mkuu mrithi wake, Nyabaganga Taraba wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba (wa pili kushoto) akiwa
katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani humo.
Wengine kuanzia kushoto waliokaa ni Katibu Tawala wa Wilaya, Shadrack
Kangese, Mkuu wa wilaya mstaafu, Hawa Ngh’umbi na Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa wilaya hiyo, Wilson Nyamunda.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...