Kocha mpya wa  Manchester United, Jose Mourihon.
 Kocha mpya wa  Manchester United, Jose Mourihon akisimamia mazoezi ya Timu hiyo ikiwa ni maandalizi kuelekea msimu Mpya wa ligi ya Uingereza.
Wachezaji wa timu ya Manchester United wakijinoa kwaajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi kuu ya Uingereza (EPL) katika viwanja vya Old Trafford jijini London nchini Uingereza.

MTANDAO wa Manchester United umeweka wazi picha za mwanzo za mazoezi chini ya kocha mpya Jose Mourinho,  huku wachezaji Henrikh Mkhitaryan na Eric Bailly walikuwa miongoni mwa wachezaji walioanza mazoezi na kikosi hicho  pamoja na beki  kinda mwenye umri wa miaka 18 Axel Tuanzebe ambaye yupo kwenye mikakati ya kocha huyo na Tyrell Warren (17) ambaye ni beki wa kulia.

Mourinho ameanza mazoezi na wachezaji 23 huku Ibrahimovic akiwa bado hajajiunga na kikosi hicho ila ameweka wzi msimamo wake kuwa Manchester siyo timu ya kubeza ni ya kipekee na kwa aina ya wachezaji vijana aliokuwa nao watakuja kuwa moto wa kuotea mbali baadae.

Mafunzo kikosi:
Makipa:
 Joel Pereira, Sam Johnstone, Dean Henderson

Watetezi:
 Antonio Valencia, Guillermo Varela, Timothy Fosu-Mensah, Eric Bailly, Phil Jones, Daley Blind, Axel Tuanzebe, Luke Shaw, Tyler Blackett

Viungo:
 Michael Carrick, Ander Herrera, Jesse Lingard, Juan Mata, Ashley Young

Washambuliaji:
 Henrikh Mkhitaryan, Memphis, James Wilson, Will Keane, Andreas Pereira, Adnan Januzaj.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2016

    Old Trafford Manchester jijini London, jiografia ulale mahala pema peponi

    Training grounds re actually in Carrington not OT

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...