Mkuu
wa Mkoa wa Kagera, Meja Generali (Mstaafu), Salum Kijuu akizungumza
wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Uimarishaji wa mifumo ya sekta za Umma
(PS3) unaotekelzwa katika mikoa 13 ya Tanzania bara kwa ushirikiano wa
baina ya Shirika la Misaada la Kimataifa la Marekani (USAID) na
Serikali ya Tanzania. Mradi huo utazihusisha Halmashauri 93 katika mikoa
hiyo.
Mtaalam
wa fedha wa mreadi wa PS3 ambaye ndie msimamizi wa uzinduzi huo Mkoani
Kagera, Abdul Kitula akielezea maeneo mbalimbali ambayo mradi huo
utahusika na kufanya kazi.
Kitula alisema PS3
inalenga kuunda ushirikiano na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya
kuimarisha mifumo ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora,
rasilimali watu, fedha, utoaji wa taarifa, na tafiti tendaji.
Wakuu wa Wilaya za mkoa wa Kagera wakifuatilia uzinduzi huo.
Mratibu
wa Mradi wa PS3 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI), Bertha Swai akijibu na kutolea ufafanuzi baadhi ya maswali
yaliyoulizwa na washiriki.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...