Msimamizi wa Ushauri na Utafiti (PSPTB), Amos Kazinza akitoa mada LEO katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Kulia ni Mkuu wa Idara ya Ugavi, Pindani Nyalile akiwa kwenye semina hiyo. Semina hiyo imelenga kutoa mafunzo kwa watendaji wa MNH ili waweze kuzingatia taratibu na sheria za manunuzi. Wakurugenzi na wakuu wa idara wa MNH wametakiwa kutoa haki wakati wa kutoa zabuni. Pia, wameshauriwa kutonunua bidhaa zilizopo chini ya kiwango. 
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru (kulia) akifuatilia mada katika semina hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha, Gerald Jeremia akiwa katika semina hiyo LEO. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Aminieli Aligaesha akisikiliza jambo kwenye semina hiyo.
              Baadhi ya wakurugenzi na wakuu wa idara wakiwa kwenye semina                                 hiyo ya siku tatu iliyoanza LEO katika hospitali hiyo.
Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...