Na Adili Mhina

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalim amesema kuwa serikali iko mbioni kupeleka bungeni muswada wa marekebisho ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ili kutotoa mwanya kwa watoto wa kike kuolewa katika umri wa chini ya miaka 18.

Mhe. Ummy ameyasema hayo katika sherehe za kuadhimisha siku ya idadi ya watu duniani ambaazo huadhimishwa tarehe 11 Julai kila mwaka.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim (Mb) akitoa hotuba yake katika sherehe za kuadhimisha siku ya idadi ya watu zilizofanyika Julai 11 katika viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.

Kwa hapa nchini, sherehe hizo zimefanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kuhudhuriwa na wawakilishi mbalimbali kutoka serikalini, mashirika ya umoja wa mataifa pamoja na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.

Katika hotuba yake kwenye sherehe hizo zilizotawaliwa na kauli mbiu ‘wezesha msichana afikie ndoto zake’, Waziri Mwalim alisema serikali imejipanga vizuri kuhakikisha haki za watoto wa kike zinalindwa hivyo ni lazima kila mwanachi aelewe umuhimu wa kumlinda mtoto wa kike na kuachana na mila potofu.
Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya idadi ya watu duniani.

“Hata hivyo pamoja na sheria hizi nzuri tatizo la mimba za utotoni halitokwisha kama jamii haitabadilika kuhusu mtizamo hasi walio nao baadhi ya watu kuhusu wasichana. Watoto wakike wanatakiwa kuwa shuleni na kupata taarifa sahihi za msingi kuhusu afya zao na kuondoa unyanyapaa, “ alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy alieleza kuwa kulingana na sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Tanzania inakadiriwa kuwa na wasichana wadogo milioni 3.4 (wenye umri kati ya miaka 13 hadi 19) sawa na asilimia 7.6 ya watanzania wote na hivyo idadi hii haiwezi kupuuzwa katika mipango mbalimbali ya Taifa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mhe. Ummy Mwalim akipata maelezo kutoka kwa moja ya washiriki wa maadhimisho ya siku ya idadi ya watu duniani.

Waziri Ummy pia alitoa pongezi kwa Tume ya Mipango hususani kwa Kaim katibu Mtendaji Bibi Florence Mwanri kwa jitihada zake za kuhakikisha masuala ya watoto yanaendelea kutambuliwa zaidi na yanafungamanishwa na maendeleo ya uchumi wa nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...