WAFANYAKAZI wa ngazi ya zahanati wanaoongoza kubaki katika vituo vya vya kazi kuliko wa ngazi zingine zote

Hayo yamesemwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mkapa, Dk. Ellen Mkondya Senkoro wakati akizungumza wadau wa afya wa kutoka mkoa Mbalimbali hapa nchini katika warsha kuwasilisha matokeo ya Tathmini mbalimba za Rasilimali watu katika sekta ya Afya zilizofanywa na taasisi ya Benjamini Mkapa leo jijini Dar es Salaam leo.

amesema kuwa Taasisi ya Mkapa imetoa matokeo ya Tathmini za rasilimali watu ambazo zimefanywa katika sekta ya afya katika Halmashauri 17 za Wilaya zilizopo mikoa 7 ya Tanzania Bara.  

Dk. Ellen  amesema kuwa  Sababu zinachangia kubaki kwenye vitu vyao kazi ni pamoja na Kupewa motisha ya posho ya kujikimu na nyumba ya kuishi karibu na vituo vyao, Kupewa ardhi kwa gharama nafuu ikiwa na viongozi wa halmashauri wanawasaidia watumishi wa Afya kujiwekea malengo ya utendaji kazi wao.

Hata hivyo Dk. Ellen ameomba Mfumo wa OPRAS ufanyiwe meboresho ili uendane na baadhi ya kada katika sekta ya Afya. 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mkapa, Dk. Ellen Mkondya Senkoro akizungumza na wadau wa afya wa kutoka mkoa Mbalimbali hapa nchini katika warsha ya kuwasilisha matokeo ya Tathmini mbalimba za Rasilimali watu katika sekta ya Afya zilizofanywa na taasisi ya Benjamini Mkapa leo jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi wa shirika linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani( UNFPA) hapa nchini, Dk. Natalia Kanem akizungumza na wadau wa afya katika warsha ya kuwasilisha matokeo ya Tathmini mbalimba za Rasilimali watu katika sekta ya Afya zilizofanywa na taasisi ya Benjamini Mkapa leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wadau wa afya Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mkapa, Dk. Ellen Mkondya Senkoro katika warsha ya kuwasilisha matokeo ya Tathmini mbalimba za Rasilimali watu katika sekta ya Afya zilizofanywa na taasisi ya Benjamini Mkapa leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...