Wajasiriamali
wakubwa kwa wadogo wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia fursa
zilizopo ili waweze kuwezeshwa mitaji ili wawekeze katika shughuli za
maendeleo ili kupunguza tatizo la ajira hapa nchini na kusaidia juhudi
za serikali na wadau kuleta maendeleo hapa nchini.
Hayo
yalisemwa na Balozi wa Japan hapa nchini Bwana Masaharu Yoshida
alipokua akifungua semina ya wadau wa maendeleo iliyojadili uwezeshaji
wa mitaji kwa wajasiriamali kwa ajili ya shughuli za maendeleo
iliyofanyika jana (5/6/2016) jijini Dar es Salaam.
Semina
hiyo iliyoandaliwa na shirika la ushirikiano na maendeleo la Japan
(JICA) pamoja na taasisi ya sekta binafsi hapa nchini (TPSF)
ilihudhuriwa na mashirika na taasisi za kifedha pamoja na wajasiriamali
kutoka sekta binafsi.
Mkurugenzi wa kitengo cha Africa wa JICA, Hideki Watanabe akielezea Jinsi JICA wanavyofanya shughuli za Maendeleo Afrika
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti, watoa mada walionesha kuwa kuna fursa kubwa kwa
watanzania wote walioamua kuwa wajasiriamali kwa kufungua viwanda vidogo
kwa vikubwa, wakulima na wafanyabiashara kutumia mashirika na taasisi
za fedha kujipatia mikopo nafuu ili kuwezesha kukuza biashara na viwanda
vyao na wanaweza kulipa kwa muda mrefu kwa riba nafuu.
Semina
hiyo ilibainisha kuwa changamoto kubwa ni kutokua na taarifa kwa
watanzania wengi na hivyo kuogopa kuwekeza kwa kutumia taasisi za fedha
jambo lililoungwa mkono na washiriki wengi kwani imebainika kuwa ni
asilimia 16 tu ya watanzania wanatumia huduma za kibenki hivyo wameaswa
kubadilika waweze kunufaika na mitaji ambayo ipo lakini hakuna
wanaokidhi vigezo ambapo wanaofuatilia na kunufaika ni watu wachache.
Mwavuli
wa wajasiriamali wa Namaingo (Namaingo Business Agency) ni moja ya
taasisi zilizohudhuria na ziliahidiwa kupewa ushirikiano na wadau wote
wa kuwasaidia kufikia malengo yao kwani mitaji ipo na Namaingo inakidhi
vigezo vyote vya kukopesheka kwani mpango kazi wake uko kitaalamu na
ushiriki wa serikali na taasisi zake unaifanya iwe mkombozi kwa
watanzania wengi maskini.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...