Na  Bashir   Yakub.

Mtu akimuumiza mwingine na  aliyeumizwa  akapata  jeraha  linalosababisha  alazwe  hospitali  au  asilazwe   lakini  aendelee  kuishi  na  jeraha  lake  hilo, Swali litakuwa  je  mtu  huyo  akifa  baada  ya  miezi  sita,  saba ,  kumi  au  zaidi   tokea  siku  alipoumizwa   kifo  chake  kitakuwa  kimesababishwa na yule  aliyemuumiza ?.

1.NINI  MAANA  YA  KUSABABISHA  KIFO.

Kusababisha  kifo   kunaweza  kuelezwa   katika  namna  nne  tofauti.  Na  hii  ni kwa  mujibu  wa  Sura  ya 16, kifungu cha  203, Kanuni  za  adhabu.

( I ) Mtu  amemtia  jeraha  mtu  mwingine.  Na  kutokana  na  jeraha  hilo  mtu  huyo  anakufa.  Haijalishi  amekufa  akiwa  anapata  matibabu  au  laah.  Na  haijalishi  kama  matibabu  hayo  yalikosewa  au  laah. La  msingi  ni  kuwa  matibabu  hayo  yalifanywa  kwa nia   njema na  hiyo  yatosha  kusema fulani  aliyesababisha  jeraha ndiye  huyohuyo  aliyesababisha kifo.

( ii ) Pengine  ni  pale ambapo  mtu  anamlazimisha  mtu  mwingine  kwa  kumtishia  akimtaka  atende  tendo   ambalo   linasababisha  kifo  cha  mtu  mwingine.  Mtu  huyo  aliyetishia  atahesabika  kusababisha  kifo.

(iii) Zaidi,  kutotekeleza  wajibu  ambako  kunapelekea  kifo  nako  ni kusababisha  kifo.  Kwa  mfano   daktari  aliyetakiwa  kumpokea  mgonjwa  na  kumtibia akishindwa  kufanya  hivyo  na  mgonjwa  akafa  basi  atakuwa  amesababisha  kifo.

( iv) Pia  ikiwa  mtu  ana jeraha   au  ugonjwa  ambao  kwa  vyovyote  vile  ungemsababishia  kifo  lakini  akatokea  mtu  mwingine  akatenda  tendo  ambalo  linasababisha  mgonjwa  afe  haraka  basi    mtu  huyo  aliyetenda  anahesabika  kusababisha  kifo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...