Na Bashir Yakub.
Mtu akimuumiza mwingine na aliyeumizwa akapata jeraha linalosababisha alazwe hospitali au asilazwe lakini aendelee kuishi na jeraha lake hilo, Swali litakuwa je mtu huyo akifa baada ya miezi sita, saba , kumi au zaidi tokea siku alipoumizwa kifo chake kitakuwa kimesababishwa na yule aliyemuumiza ?.
1.NINI MAANA YA KUSABABISHA KIFO.
Kusababisha kifo kunaweza kuelezwa katika namna nne tofauti. Na hii ni kwa mujibu wa Sura ya 16, kifungu cha 203, Kanuni za adhabu.
( I ) Mtu amemtia jeraha mtu mwingine. Na kutokana na jeraha hilo mtu huyo anakufa. Haijalishi amekufa akiwa anapata matibabu au laah. Na haijalishi kama matibabu hayo yalikosewa au laah. La msingi ni kuwa matibabu hayo yalifanywa kwa nia njema na hiyo yatosha kusema fulani aliyesababisha jeraha ndiye huyohuyo aliyesababisha kifo.
( ii ) Pengine ni pale ambapo mtu anamlazimisha mtu mwingine kwa kumtishia akimtaka atende tendo ambalo linasababisha kifo cha mtu mwingine. Mtu huyo aliyetishia atahesabika kusababisha kifo.
(iii) Zaidi, kutotekeleza wajibu ambako kunapelekea kifo nako ni kusababisha kifo. Kwa mfano daktari aliyetakiwa kumpokea mgonjwa na kumtibia akishindwa kufanya hivyo na mgonjwa akafa basi atakuwa amesababisha kifo.
( iv) Pia ikiwa mtu ana jeraha au ugonjwa ambao kwa vyovyote vile ungemsababishia kifo lakini akatokea mtu mwingine akatenda tendo ambalo linasababisha mgonjwa afe haraka basi mtu huyo aliyetenda anahesabika kusababisha kifo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...