MFUKO wa Pensehni wa PSPF, umeendelea kusajili wanachama wapya kupitia
Mpango wa Uchangiaji wa Hiari wa PSS, wakati wa Maonyesho ya taasisi na
makampuni ya kutoa huduma yaliyoandaliwa na Kampuni ya simu za mikononi,
Airtel na kwenda na jina la Airtel Bazzar na kufanyika makao makuu ya
kampuni hiyo Morocco jijini Dar es Salaam, Agosti 12, 2016.
Akizungumza
na waandishi wanhabari kwenye banda la Mfuko huo, Mkuu wa Kitengo cha
Usajili nwa Wanachama cha Mfuko huo, Bw. Msafiri S. Mugaka, alsiema,
PSPF kupitia mpango wake wa PSS, imefanikiwa kusajili wanachama wapya
kadhaa, ambayo ilikuwa ni moja ya huduma walizokuwa wakizitoa kwenye
maonyesho hayo ya siku moja.
"Pia wanachama wetu waliweza kuja na
kupatiwa huduma za taarifa za michango yao, wanawezaji kufaidika na
mafao mbalimbali ya yatolewayo na Mfuko kama vile fao la Elimu, Uzazi,
mikopo kwa wafanyakazi wapya, na mafao mengine kadhaa,"alisema.
Maonyesho
hayo yalishirikisha makampuni kadhaa ya kibinafsi na taasisi za umma na
yalilenga kuwakutanisha wateja wa Airtel, na taasisi hizo ikiwa ni
pamoja na wafanyakazi wenyewe wa Airtel kutembelea taasisi hizo na
kupatiwa huduma mbalimbali wakiwa hapo hapo kazini.
Mkuu wa kitengo cha kuandikisha wanachama cha Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Msafiri S. Mugaka, akiwapatia maelezo wanachama hawa wa PSPF, kuhusu mafao na faida nyingi ambazo mwanachama anaweza kupata ikiwa ni sehemu ya huduma zitolewazo na Mfuko.
Elimu ikiendelea kutolewa kuhusu huduma za Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kwa wananchi waliotembelea banda la Mfuko huo
Penzila Kaisi (kulia), Afisa Matekelezo msaidizi wa PSPF, akimuelimisha mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo ili kujua shughuli zake.
Angelina akitoa somo kwa mwananchi huyu.
Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, Maseka Kadala, (kulia), akimsikilzia kwa makini mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo ambapo baadaye alijiunga baada ya kuelewa huduma za Mfuko huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...