Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akipokea msaada wa chakula kutoka kwa Mhe. Leontine Nzeyimana, Waziri wa Afrika Mashariki wa Burundi ikiwa ni msaada kutoka Serikali ya Burundi kwa ajili ya Waathirika wa tetemeko la ardhi huko Mkoani Kagera. Msaada huo ni pamoja na mchele tani 100, sukari tani 30, mahindi tani 50 na majani ya chai tani 3. 
Mhe. Dkt. Kolimba akitoa shukrani za dhati kwa niaba ya Serikali kwenda Serikali ya Burundi baada ya kupokea msaada huo wa chakula. 
Mhe. Dkt. Kolimba akiwa katika picha ya pamoja Mhe. Nzeyimana na wadau wengine. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salim Mustafa Kijuu akifuatiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...