Na Bakari Issa Madjeshi,
Globu ya Jamii

Serikali imeagiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya Kusimamia zoezi la kuondoa makazi ya Watu waliojenga karibu na Shule za Msingi, Sekondari, Zahanati, Vituo vya Afya na Maeneo ya Masoko kwa kile kilichoelezwa kuwa ni usumbufu na kuondoa utulivu katika maeneo hayo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mhe. George Simbachawene (pichan) amesema katika maeneo hayo kuna uvamizi tofauti ikiwa ujenzi wa Nyumba za Kufanyia biashara.
Mhe Simbachawene amesema upo uvamizi mwingine ambao ni uporaji wa ardhi iliyotengwa kwa ajili ya Shule, Zahanati mijini na vijijini.
Mhe. Simbachawene ametoa wito kwa wananchi kushirikiana na serikali kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa juu ya Uvamizi huo kwa kuonyesha alama za mipaka ya maeneo hayo.
‘’Wakurugenzi wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa waanzishe zoezi la kubainisha mipaka ya asili ya maeneo yote na kuyapima kuhakikisha yana Hati Miliki’’, amesema Mhe. Simbachawene

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...