NAHODHA wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC,
John Bocco ‘Adebayor’, amewatakia mashabiki wa timu hiyo kheri ya mwaka mpya
‘2017’ unaoanza leo saa 6.00 usiku huu huku akiwashukuru kwa sapoti yao
waliyoionyesha mwaka huu.
Bocco ametoa kauli hivi karibuni mara baada ya kumalizika kwa
mchezo uliopita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) dhidi ya Tanzania Prisons
walioifunga bao 1-0, huku akifanikiwa kutupia bao hilo pekee lililorudisha
morali ndani kikosi hicho baada ya kutofanya vizuri kwenye mechi mbili za
ufunguzi wa mzunguko wa pili walipocheza ugenini na African Lyon (0-0) na
Majimaji (1-1).
“Kwanza tunawashukuru mashabiki wetu kwa uvumilivu
waliouonyesha, kwa sapoti waliotupa katika kipindi chote kigumu tulichopitia,
kama wachezaji na timu kwa ujumla tunawaomba waendelee kuwa na moyo huo huo na
pia tunawatakia kheri ya mwaka mpya (2017) na wamalize mwaka huu vizuri,
tuendelee kuwa pamoja ili kuisaidia timu yetu iweze kufanya vizuri,” alisema
Bocco wakati akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz
Bocco ambaye ameipatia mafanikio makubwa Azam FC kwa mabao yake
muhimu tokea timu hiyo ikiwa madaraja ya chini hadi kupanda Ligi Kuu mwaka
2008, aliendelea kusema kuwa wamepitia changamoto nyingi sana kwa mwaka huu
unaoisha huku akidai kuwa wamejifunza kupitia hayo na wanachoangalia kwa mwaka
mpya ni kuipeleka mbele zaidi timu hiyo ili kufikia mafanikio. Kusoma zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...