Na Amina Kibwana,
Globu ya Jamii
Kituo cha radio cha Efm kwa kushirikiana na kampuni ya multichoice Tanzania kimekabidhi makapu yaliyosheheni bidhaa za vyakula sambamba na ving'amuzi na vifurushi vya mwezi mmoja kwa washindi 24 wa shindano la kapu la sikukuu kwa kusherehekea sikukuu ya krismas na mwaka mpya.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa Wilaya ya ilala Sophia Mjema ametoa shukrani zake kwa uongozi wa efm na Dstv pamoja na kuwaasa washindi wote waendelee kuangalia Dstv na kusikiliza efm ili waendelee kufaidika kwani kusikiliza redio kutawasaidia kujua mambo mbalimbali ya kijamii.
"Nashukuru uongozi wa Efm na Multichoice Tanzania kwa kuonyesha kuwajali wateja wao kwani jambo kama hili ni nadra sana kutokea."
Kwa upande wake Meneja Masoko wa Kampuni ya Multichoice Alfa Mria amesmea kuwa kampuni imeamua kuwatunuku washindi washindi hao ving'amuzi na vifurushi vya mwezi mzima vya Dstv ili kuwafanya wao na familia zao kusherehekea sikukuu ya krismas na mwaka mpya kwa furaha huku wakitazama Dstv.
" Hatujawatunuku washindi wa kapu la sikukuu tu bali tumewatunukia Watanzania kwani hivi karibuni tumeshusha bei za ving'amuzi vyetu kwa silimia 16 wakati king'amuzi cha Dstv Bomba chenye chanell zaidi ya 70 kikiwa kimepunguzwa bei hivyo hii ni zawadi kwa watanzania wote."
Shindano hili la kapu la sikukuu liliwataka wasikilizaji wa Efm kusikiliza mlio wa jingle bells uliokuwa ukizunguka kwenye vipindi tofauti kisha kutambua muda ambao mlio huo umesikika.jina la kipindi na jina la mtangazaji wa kipindi husika kilichokuwa hewani muda huo pamoja na kuangalia king'amuzi cha Dstv na kujibu maswali kutoka Multichoice Tanzania.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (katikati), akimkabidhi zawadi msanii Irene Paul.
Maelekezo ya upokeaji wa zawadi hizo yakitolewa.
DC Mjema akizungumza na wanahabari baada ya kukabidhi zawadi hizo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...