TWIGA WA KIPEKEE DUNIANI
Twiga huyu mwenye ulemavu wa ngozi ambae kisayansi anajulikana kwa jina la 'OMO' akifananishwa na SABUNI YA OMO, aligunduliwa na Dk.Derek Lee katika mbuga ya TARANGIRE,Mkoani Arusha wakati dokta huyo akifanya uchunguzi na utafiti wa wanyama mbalimbali.
Dk.Lee 'alimgundua' twiga huyu mwenye ulemavu wa ngozi kutokana na utofauti wake na twiga wenzake ambao wanapatikana katika mbuga hiyo.Twiga huyu alioneakana akiongozana na twiga wenzake sehemu mbalimbali za mbuga hiyo bila ya twiga wenzake kumshangaa wala kumtenga twiga huyu.
Mnyama huyu ni mnyama aliyetofauti sana na wanyama wenzake katika kipengele cha rangi kwani rangi yake ni ile nyeupe ya kukolea inayofanana kabisa na rangi ya binadamu mwenye ulemavu wa ngozi ingawa hali hii kitaaluma inaitwa inaitwa leuscism na siyo albinism per se
Gazeti moja la kimarekani lilitoa ripoti kwamba twiga wa aina hii yani mwenye ulemavu wa ngozi ni wachache sana hapa duniani na kama twiga huyu atatunzwa vizuri basi atakuja kuwa moja ya kivutio kikubwa sana cha utalii hapa duniani.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...