Watanzania wametakiwa kuongeza hamasa ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini ikiwemo hifadhi za Taifa ili kufurahia rasilimali walizotunukiwa na Mwenyezi Mungu.

Mchungaji Josephine Miller kutoka nchini Marekani aliyasema hayo jana wakati wa ziara yake ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti ili kujionea vivutio mbalimbali vya wanyama katika hifadhi hiyo.

Alisema alipokuwa katika hifadhi mbalimbali barani Afrika ikiwemo za Afrika Kusini na Zimbabwe, alikuwa akisikia kuhusu uzuri wa hifadhi ya Serengeti hivyo amefurahia kutembelea hifadhi hiyo akisema kwamba hilo lilikuwa ni chaguo lake la pili baada ya kuonana na watu wa bara la Afrika.

Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Kulola, alisema ni vyema Mamlaka ya Hifadhi za Taifa TANAPA ikaongeza hamasa kwa Watanzania kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kuukuza zaidi utalii wa ndani huku akiomba suala la miundombinu ya barabara kuboreshwa ili watalii.

Kumbuka Mtanzania hulipa Tsh.11,800 pamoja na VAT kwa mtu mzima ili kuingia katika hifadhi ya Serengeti. Wageni hulipa dolla 70 ikikadiliwa kuwa Tsh, laki moja na elfu hamsini na nne. Hakika watanzania wanayo furusa kubwa kutembelea vivutio vya vya utalii.
Waumini wa EAGT Lumala Mpya wakifurahia uwepo wao ndani ya hifadhi
Mchungaji Josephine Miller kutoka Marekani (kulia) akifurahia uwepo wake ndani ya hifadhi ya Serengeti. Kushoto ni Mwanahabari na Blogger wa Lake Fm Mwanza, George Binagi
Pundamilia, nyumbu na nyati wakiwa kwenye makundi ndani ya hifadhi ya Serengeti
Twiga na upendo wao, hawaachani
Ni muda wa chakula ndani ya hifadhi ya Serengeti huku pia Watalii wa Ndani na Watalii wa Nje, wakifurahia pamoja uzuri wa hifadhi ya Serengeti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...