Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amezitaka Kampuni za Mawasiliano kukamilisha taratibu za usajili katika Soko la Hisa la Dar es Salaam kwa kuuza asilimia 25 ya hisa zote kadri ya Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana inavyoelekeza mwishoni mwa mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Prof. Mbarawa ametaja kampuni hizo kuwa ni zile zenye leseni za mawasiliano zilizotolewa kabla ya tarehe 1 Julai 2016 kwa ajili ya Miundombinu ya Mawasiliano, Huduma za Mawasiliano, na Huduma za Matumizi.

“Watoa huduma wote wa Mawasiliano wajisajili na kuuza hisa zao kwa wananchi ndani ya mwezi wa Disemba”, amesema Waziri Prof. Mbarawa.
Ameongeza kuwa kwa Kampuni zilizopata leseni baada ya tarehe mosi Julai, 2016 watatakiwa kutimiza sharti hilo la kisheria kwa kipindi kisichozidi miaka miwili tangu kusajiliwa.

Waziri Prof. Mbarawa amesisitiza kuwa Kampuni zitakazokiuka Sheria hiyo zitachukuliwa hatua za kisheria kupitia kifungu cha 21 (C) cha EPOCA, 2010.
Aidha, amewataka wananchi kutumia fursa hiyo kununua hisa hizo na kuwa sehemu ya wamiliki wa makampuni ya Mawasiliano ili kuongeza kipato na kushiriki katika maamuzi ya kampuni hizo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa sheria ya EPOCA kulingana na mabadiliko yaliyofanywa katika Sheria ya Fedha No. 2 ya mwaka 2016, jijni Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...