Watumiaji wa simu za mkononi wameaswa kutokutoa namba za siri za simu zao wanapopigiwa simu au kutumiwa ujumbe mfupi yaani SMS. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Bi. Jacquiline Materu, alisema“Natoa wito kwa wateja wetu kuwa makini na matapeli wanaowapigia simu na kuwafahamisha kuwa wameshinda fedha za Promosheni ya Nogesha Upendo au bonasi ya M-Pesa. 

Vodacom Tanzania haina utaratibu wa kuwapigia simu wateja kuhusiana na mgao wa fedha za bonasi ya M-Pesa bali inatoa mgao huo kwa kadri ya mteja alivyotumia huduma hii na rekodi zote za matumizi kampuni inazo sambamba na utaratibu uliowekwa na Benki Kuu. 

Materu alisema kampuni inawapigia simu wateja wa Promosheni ya Nogesha Upendo tu na kuwajulisha kuwa wameshinda na fedha zao hutumwa moja kwa moja kwa njia ya M-pesa ndani ya masaa 48 bila kuwataka wateja hao kutoa taarifa zozote za siri juu ya namba zao. Wengine wanaowapigia simu wateja kuhusiana na bonasi ni matapeli ambao wanataka kupata namba za siri na kuwatajia kiasi gani cha fedha mlizonazo ili wapate fursa ya kuwaibia fedha,” alisema Materu.

Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Bi. Jacquiline Materu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...