Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imetoa ruksa kwa Klabu ya Yanga na Simba kutumia Uwanja mkuu wa Taifa katika michezo ya ligi kuu ya Vodacom kuanzia  kesho ambapo kutakuwa na mtanange wa baina ya timu ya Simba na Azam FC utakaopigwa kwenye dimba hilo kuanzia saa 10 jioni.

Uwanja huo wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 60,000 ulifungiwa na Serikali kumika baada ya mchezo wa Oktoba mosi baina ya Simba na Yanga kutokana na vurugu zilizosababisha uharibifu uliofanywa na mashabiki wa Wekundu hao kuvunja viti 1871.

Ofisa habari wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) Alfred Lucas imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli kwa kukubali ombi la kuwaruhusu kuendelea kutumia uwanja huo huku pia akimpongeza Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo Nape Nnauye kwa kusimamia hadi kufikia hatua hiyo.

"Serikali ya awamu ya tano ni sikivu na TFF inampongeza Rais Magufuli kwa kuruhusu mechi za ligi kuu ya kuchezwa katika uwanja wa Taifa pia Waziri Nape kwa kusimamia hadi kufikia hatua hii" alisema Lucas.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...