*Awaonya viongozi wa siasa wasiwavuruge wananchi
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameumaliza mgogoro
wa mpaka wa ardhi baina ya vijiji vya wilaya za Kiteto na Kilindi uliodumu kwa muda
mrefu.
Mgogoro huo ambao ulianza kusuluhishwa tangu
mwaka 1997, umepata suluhu kwenye mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu
na kuwajumuisha Wakuu wa Mikoa hiyo miwili, Wabunge wa Kiteto na Kilindi, wenyeviti
wa Halmashauri na madiwani wa kata mbili za mpakani pamoja na wananchi wa kata
hizo.
Waziri Mkuu pia amewataka wanasiasa na
viongozi wengine kutowavuruga wananchi na badala yake wawaongoze vizuri na
kutoa maelekezo kwa mujibu wa sheria za nchi.Ametoa
agizo hilo leo (Jumatano, Januari 18, 2017) wakati akizungumza na wananchi wa wilaya za
Kiteto na Kilindi katika kijiji cha Lembapili wilayani Kiteto, mkoani Manyara ambako
ni kuna mpaka wa wilaya hizo mbili alipokwenda kutatua mgogoro huo.
Amesema
viongozi wa wilaya hizo lazima wafuate sheria na wawaelekeze wananchi umuhimu
wa kuzingatia sheria za nchi ikiwa ni pamoja na kuheshimu mipaka iliyowekwa kwa
mujibu wa sheria ili kuepusha migogoro.
Akizungumzia
kuhusu mgogoro huo wa mpaka, Waziri Mkuu amesema nchi ilishaweka mipaka ya
mikoa na wilaya zake yote tangu zamani na kumbukumbu zipo zikiwemo za mpaka wa
wilaya hizo tangu mwaka 1961 kwa tangazo la Serikali namba 65 na
hakuna mabadiliko. Hivyo, aliwasisitiza wauheshimu na kuufuata.
Amesema
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi itakwenda
kuweka alama vizuri na viongozi wa wilaya hizo watashirikishwa. Alama hizo
zitawekwa na kifaa maalumu, hivyo amewataka wahusika watoe ushirikiano.
Waziri
Mkuu amesema katika kipindi ambacho Serikali itakuwa ikiweka alama hizo, wananchi
waendelee na shughuli zao hadi hapo zoezi litakapokamilika na wala wasibughudhiwe.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizugumza na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi (kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Joel Bendera wakiwa katika kijiji cha Lembapuli kilichopo kwenye mpaka wa wilaya ya Kiteto na Kilindi Januari 18, 2017. Mheshimiwa Majaliwa alikwenda Kiteto na Kilindi kutatua mgogoro wa mpaka unaovikabili vijiji vya Mafisa na Kijungu. Wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga na Muu wa Wilaya ya Tanga mjini , Thobias Mwilapwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akielekea kwenye moja ya jiwe la mpaka wa wilaya ya Kilindi na Kiteto wakati alipokwenda kwenye kijiji cha Lembapuli kilichopo kwenye mpaka wa Kiteto na Kilindi kutatua mgogoro wa mpaka Januari 18, 2017. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Joel Bendera na kulia kwake ni Mkuu wa wilaya na Tanga na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga Thobias Mwilapwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa watalaam wa upimaji ardhi kuhusu jiwe la alama ya mpaka wa wilaya ya Kilindi na Kiteto katika kijiji cha mpakani cha Lembapuli Januari 18, 2017. . Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Joel Bendera na kulia kwake ni Mkuu wa wilaya na Tanga na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga Thobias Mwilapwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu ramani inayoonyesha mpaka wa wilaya ya Kilindi na Kiteto katika kijiji cha mpakani cha Lembapuli wakati alipokwenda kutatua mgogoro wa mpaka kati ya wialya hizo Januari 18, 2017. Mheshimiwa Majaliwa apia alifuatana na Mawaziri , William Lukuvi wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi na George Simbachawene wa Ofisi ya Rais- TAMISEMI.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...