Na Bashir Yakub. 

Yafuatayo ni maneno/taarifa/maudhui ya msingi yanayotakiwa kuwa kwenye wosia . Taarifa yoyote kati ya hizi ni ya muhinu na inacho kitu cha msingi na cha kisheria inachosimamia na kulinda. Maana yake ni kuwa kukosekana kwake kutaathiri wosia wako kwa namna moja au nyingine.

( a ) Anza kwa kuandika kichwa( heading). Kichwa utaandika kawaida kama unavyoandika kichwa cha barua au taarifa nyinginezo. Mfano “WOSIA” au “ WOSIA WANGU MIMI PASCHAL STEVEN MUTIGANZI”, vyovyote kitakavyoandikwa muhimu kiwepo kichwa.

( b ) Kinachofuata baada ya kichwa ni sentensi muhimu sana. Ni sentensi inayolenga kuondoa utata mbeleni.

Mfano ; “ HUU NI WOSIA WANGU NA WA MWISHO MIMI PASCHAL STEVEN MUTIGANZI”.

Ni sentensi inayoazimia kuwa hakuna wosia mwingine baada ya huo. Ni sentensi inayolenga kufuta/kuondoa aina yoyote ghushi.

( c ) Kinachofuata ni kipengele ambapo mtoa wosia/mwandika wosia anajitambulisha kwa majina kamili, anuani na tarehe ya kutoa/kuandika wosia. Anuani ijieleze vizuri. Isiwe tu P.O. BOX… ikaishia hapo. Ieleze namba ya nyumba kama ipo, mtaa, kata, wilaya na mkoa. Na anuani nzuri ya kuweka ni ile ya pahala yalipo makazi yako ya kudumu wewe mtoa wosia. Ikiwa unayo makazi mawili ya kudumu kwa wale wa mitala basi chagua mojawapo.

Mfano: “WOSIA HUU UMEANDIKWA LEO TAREHE 13 / 2 / 2017 NA MIMI PASCHAL STEVEN MUTIGANZI WA NYUMBA NAMBA 13 , MTAA WA MWINJUMA, KATA MWANAYAMALA , WILAYA YA KINONDONI, MKOANI DAR ES SALAAM, wa S.L.P 100 .

( d ) Andika sentensi ya kuvunja wosia nyingine zilizopita. Hii ni pale ambapo umeandika wosia mpya na kufuta ule wa nyuma. Lakini hata kama haujawahi kuandika wosia ila sasa ndio unaanza basi hakuna ubaya pia ukiweka sentensi hiyo.

Mfano ; “WOSIA HUU UNAFUTA WOSIA NYINGINE ZOTE NILIZOWAHI KUTOA/KUANDIKA HUKO NYUMA”.

( e ) Kinachofuata ni kipengele kinachotaja orodha ya mali ulizonazo. Habari si tu kutaja mali, bali pia ni kuzichambua mali hizo na kutaja pahala zilipo kila moja. Mali utazitaja kwa namba. Namba 1….2……3…..n.k. Mfano ; “JUMLA YA MALI NILIZONAZO NI, 1. NYUMBA NAMBA 13 , ILIYOPO MTAA WA MWINJUMA, KATA MWANAYAMALA , WILAYA YA KINONDONI, MKOANI DAR ES SALAAM. 2. GARI…..”( taarifa za gari au mashine yoyote zitajwe kama ilivyo kwenye kadi yake ya usajili)……( endelea kutaja mali )

( f ) Kinachofuata ni kipengele kinachotaja orodha ya warithi/wanufaika wa mirathi. Wataje kwa majina yao yote.
Mfano; “WARITHI WANGU KATIKA WOSIA HUU NI 1………………………..2……………………………3…………………..”n.k.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...