Mabingwa wa soka barani Afrika Mamelodi Sundowns FC ya Afrika Kusini wanatarajiwa kuwasili nchini mwisho wa mwezi huu kwa mwaliko wa klabu ya African Lyon. 
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa  African Lyon, Rahim Kangezi, Mamelodi wanatarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam Januari 30, 2017 na kucheza michezo miwili ya kirafiki na Simba SC na Yanga.
 “Mamelodi wanakuja Tanzania kuiunga mkono Tanzania katika kampeni yake ya “LINDA TEMBO WETU” ambayo ni mahususi kupiga vita ujangili na biashara haramu ya pembe za tembo. 
Kangezi amesema mchezo wa kwanza Mamelodi watacheza na February 1, 2017 na Simba na February 3, 2017 watachuana na Yanga.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...