Na Humphrey Shao ,Globu ya Jamii

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi, Marcelin Ndimbwa amewapongeza wakuu wa idara wote wateule waliopitishwa na baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo.

Ndimbwa alichukua fursa hiyo mara baada ya wakuu hao kupata baraka ya baraza la madiwani wilayani humo.

“ Nina imani kubwa na ninyi, pia wananchi wa Malinyi wana imani kubwa Sana na ninyi. Tekelezeni wajibu wenu kwa kufuata (STK) zaidi Sana tunzeni nidhamu ya Hali ya juu, sio kwa mkurugenzi na m/kiti Bali kwa wananchi tena wale wa hadhi ya chini kabisa, Maana ndo waliotoa dhamana hiyo kwenuNami kwa niaba yao nimekupeni kamisheni”.

Amesema anawategemea Sana kufikia na kutimiza kile alichokikusudia kuwapa wananchi kupitia Ilani ya CCM chini ya Rais Dk John Pombe Magufuli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...