Msemaji wa Polisi, Advera Bulimba – ACP
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu ametuma
timu ya Maofisa wa Polisi ikiongozwa na
Kamishna wa Polisi Jamii Mussa Alli Mussa kwenda Zanzibar kushughulikia kero na
malalamiko ya wananchi juu ya vitendo vya udhalilishaji na ukatili kwa watoto/wanawake
ambavyo vimekuwa vikiripotiwa mara kwa mara.
Timu hiyo imepewa jukumu la kuchunguza vitendo hivyo vya
udhalilishaji na kiini chake na hatimaye kuja na mpango mkakati wa kuzuia
vitendo hivyo ikiwemo kuwakamata wahusika
na kuwafikisha mahakamani.
IGP Mangu amewataka wananchi wa Zanzibar, Taasisi za
kiserikali na Taasisi za kiraia zilizopo Zanzibar kutoa ushirikiano kwa timu
hiyo ili kukomesha vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya Watanzania.
Imetolewa na:
Advera John Bulimba - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...