Sehemu ya uwanja wa klabu ya Manchester United Old Trafford
ulishika moto asubuhi ya leo kabla vikosi vya zimamoto kufika na kuuzima.
Shuhuda wanasema walianza kuona moshi mkubwa ukifuka katika jukwaa la kusini la uwanja huo maarufu
liitwalo Sir Bobby Sharlton Stand.Klabu ya Manchester united ilisema katika twitter yake kuwa moto
mdogo uliosababishwa na hitilafu ya umeme ulizuka kwenye moja ya lifti na
wazima moto waliitwa na kufanikiwa kuuzima. Hakuna madhara makubwa yaliyotokea.
Vikosi vya zimamoto vikiwa vimeudhibiti moto huo
Jukwaa ulikozukia moto huo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...