Na Zuena Msuya, Mbeya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali ( PAC) imetoa miezi sita kwa Taasisi  na Mashirika yote kulipa madeni ya ankara wanayodaiwa na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) na endapo watashindwa kufanya hivyo watakatiwa huduma hiyo.
Agizo hilo limetolewa mkoani Mbeya na Mwenyekiti wa Kamati ya PAC , Livingtone Lusinde wakati wa ziara ya Wajumbe wa Kamati hiyo wakati wa kukagua matumizi halisi ya fedha za Serikali katika kutekeleza Miradi ya Umeme Vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati wa Vijijini( REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme nchini Tanesco.
Lusinde alisema Tanesco imekuwa ikishindwa kutimiza majukumu yake kutokana na kukosa fedha za kutosha kujiendesha na hivyo kuwakosesha wananchi hudumu muhimu ya umeme katika maeneo mbalimbali .
" Tanesco imetapakaa nchi nzima, lakini haiwezi kutoa huduma bora za uhakika kwa wateja wake katika maeneo yote hayo kutokana na miundominu mibovu na kutomfikia mteja kwa wakati kwa vile tu hawana fedha", alisema Lusinde.
 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali( PAC), wakielezwa  na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani( katikati) namna ambavyo kifaa maalum kinachofahamika kama umeme tayari( UMETA) umeme tayari kinavyofanya kazi,
 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC), wakiwa katika ziara ya kukagua matumizi halisi ya fedha za Serikali katika utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini.
 Wafanyakazi wa Kampuni ya JV State Grid wanaotekeleza Miradi ya Umeme Vijijini katika wakiendelea na kazi ya kujenga miundombinu ya Umeme Vijijini katika kijiji cha Masukulu wilayani Rungwe.
 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC), wakiwa katika ziara ya kukagua matumizi halisi ya fedha za Serikali katika utekelezaji wa Miradi ya Umeme Vijijini.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani(kulia), Mwenyeketi wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali( PAC) Livingstone Lusinde (katikati) wakisaini vitabu vya wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, wakati wa ziara ya kukagua miradi ya umeme vijijni wilayani humo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...