Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu (kulia) akizungumza wakati wa mkutano wake na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania, Profesa Sospeter Muhongo (katikati). Mkutano huo ulijadili masuala mbalimbali mojawapo ikiwa ni uboreshaji wa Bomba la Mafuta Ghafi la TAZAMA. Kushoto ni Balozi wa Tanzania Nchini Zambia, Balozi Grace Mujuma.
 Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu (kushoto) akizungumza jambo Ikulu ya Zambia Jijini Lusaka mara baada ya kumaliza mkutano wake na Ujumbe kutoka Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto kwake). Kulia ni Balozi wa Tanzania Nchini Zambia, Balozi Grace Mujuma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Tanzania, Profesa Justin Ntalikwa.
 Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu (kushoto) akifurahia jambo na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania, Profesa Sospeter Muhongo mara baada ya kumalizika kwa mkutano uliofanyikia Ikulu ya Zambia.
Rais wa Zambia, Mhe. Edgar Lungu (wa tatu kushoto mstari wa nyuma) katika picha ya pamoja na Ujumbe kutoka Tanzania na Baadhi ya Mawaziri wa nchini Zambia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...