Na.Vero Ignatus, Arusha.
Mkuu
wa mkoa wa Arusha Mashaka Mrisho Gambo amefungua Kongamana kutoa
taarifa ya maendeleo katika mkoa wa Arusha ambapo kongamano hilo
limewashirikisha wadau wa habari katika kuangalia na kutafakari na
kupitia pamoja na kuangalia mpango mkakati wa maendeleo katika mkoa.
Gambo
amesema kuwa kongamano hilo lina lengo la kutoa mrejesho kwa Watanzania
kupitia waandishi kwa kipindi cha miezi sita ,na kuangalia mambo gani
serikali ikiyapa kipaumbele itaondoa changamoto mbalimbali katika jamii
kwa ujumla.
Aidha amesema kuwa utekelezaji wa shughuli za
kiserikali katika mkoa wa Arusha kwa kipindi cha miezi sita hadi kufikia
desemba 2016 umekuwa na mafanikio makubwa ,ambapo amesema kuwa hii ni
kutokana na utamaduni wa kufanya na kutekeleza majukumu ya kazi kwa
vitendo.
Amesema utekelezaji huo umechangia katika kuboreka kwa
maeneo mbalimbali ya sekta muhimu katika kukuza uchumi katika mkoa hasa
pato la mkoa na wananchi moja kwa moja.
“Katika kipindi
hiki,miradi mingi ya maendeleo imetekelezwa na kupewa kipaumbele cha
kutosha hivyo kwa namna moja kutekeleza mkakati wa Taifa wa kukuza
uchumi na kuondoa umaskini (MKUKUTA II)katika mkoa na taifa kwa
ujumla”alisema Gambo.
Amesema kuwa Mkoa umesimamia utekelezwaji wa shughuli za serikali na kushuhudia mafanikio katika sekta zakilimo,afya,maji,barabara,mofugo,maliasili na nyinginezo kama takwimu zilivyowasilishwa .Amesema kuwa serikali imejipanga kuhangaika na wale wote ambao wanachochea migogoro kwa wananchi na kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi hatutawafumbia macho.
Mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo akiingia ukumbini tayari kwa kuanza rasmi kwa kongamano na waandishi wa habari na wadau mbalimbali wa maendeleo katika mkoa wa Arusha.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika kongamano hilo lililoitishwa na mkuu wa mkoa wa Arusha ili kuangalia na kujadili maendeleo ya mkoa kwa ujumla.
Wa kwanza kushoto ni mwandishi wa habari wa gazeti la mwananchi Mussa Juma ,akifuatiwa na Omary Moyo wakiwa katika kongamano hilo.
Mgeni rasmi mkuu wa mkoa pamoja na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari waliohudhuria kongamano hilo.Picha na Vero Ignatus Blog.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...